Tuesday, December 10, 2024

MFUGAJI ADAIWA KUAWA KIKATILI KITETO KISHA MIFUGO YAKE KUCHUKULIWA

Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Waziri Athumani Sango, maarufu Waziri Fonyoo miaka (39) mkazi wa Sunya amedaiwa kukutwa porini ameuawa na watu wasiojulikana akiwa na majeraha ya kukatwakatwa na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake

Imeelezwa mtu huyo alikuwa ni mchungaji wa mifugo, tukio hilo limetokea leo Dec 10.2024, na kwamba mmiliki wa mifugo hiyo  yeye anajulikana kwa jina la Hassani Ngor Kinyemba (22)

Imeelezwa mpaka sasa wananchi  wanaendelea kutafuta mifugo hiyo porini ambapo chanzo cha habari hizi kinasema watuhumiwa wametoweka na mifugo hiyo na wanahisi wao ndio wamefanya tukio hilo.

Chanzo cha habari hizi kinasema mwili wa mmarehemu umechukuliwa na  kuhifadhiwa  Kituo cha afya Sunya huku wananchi hao wakiomba Jeshi la Polisi kuungana pamoja kuwasaka wahalifu hao.

Mudisha tv tunaendelea kumtafuta kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Manyara kuhusu tukio hili na mara baada ya kumpata tutakuja na habari hizi zaidi.


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DED HANANG AKUTANA NA WADAU WA STAKABADHI GHALANI

DED HANANG AKUTANA NA WADAU WA STAKABADHI GHALANI Na, Mudishatv blog Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Teresia Irafay,...

Popular Post