Na Mohamed CHUMVI
Mgogoro wa mpaka kati ya wilaya ya Kiteto eneo la Lembapuli na Wilaya ya Kilindi eneo la mafisa unanukia.
Wananchi wanaoishi mpakani mwa wilaya hizo wamejawa na hofu baada ya kudaiwa kuibuka baadhi ya wananchi kutembea na silaha huku kukiwa na vitishi
Wananchi hao wanagombea ardhi kwa ajili ya shughuli za kiuchumi ambapo mpaka unatajwa kuwa chanzo cha mgogoro huo
"Wananchi wa mafisa wanatembea na silaha (bunduki) sisi Kiteto tulishapokonywa silaha zetu siku nyingi hivyo tunashindwa kujil8nda" kimesema chanzo cha habari hizi
"Tunatii sheria Kiteto lakini wenzetu hawatii na wanekuwa tishio sasa wanavamia maeneo ya Kiteto Lembapuli wakitokea mafisa kwa ajili ya kulima"amesema
Kwa upande wa wananchi wa mafisa ambao ni wakulima wamesema wananchi wa Kiteto jamii ya maasai wanawakataza kufanya shughuli za kilimo kwenye maeneo yao
"Hawa wenzetu wa Kiteto maasai eneo la Lembapuli ni jeuri sana wao wanadai maeneo tunayolima miaka yote kuwa ni yao na wanatukataza wanatupiga na silaha za jadi" amesema mmoja wa wananchi Kilindi
Mwisho

No comments:
Post a Comment