Wednesday, December 25, 2024

RAIS DKT SAMIA ASIKIA KILIO CHA MTOTO MANYARA MWENYE TATIZO LA SARATANI


Na Mohamed Chumvi

Hatimaye Rais Samia Suluhu Hassan amesikia kilio cha mtoto HUSSEIN(16) mwenye tatizo la saratani ya kichwa na kuagiza afikishwe hosp ya Benjamini Mkapa kwa matibabu

Awali mtoto huyo alirejeshwa nyumbani baada ya wazazi wake kukosa fedha za matibabu hali iliyotishia ustawi wa maisha yake

Mtoto HUSSEIN ambaye wazazi wake ni wakazi wa Babati vijijini mkoani Manyara, alipata tatizo la saratani ya Kichwa miaka michache iliyopita na kutishia maisha yake.

Akizungumza na Mudisha tv Dr. Humber BMH wa hospitali ya Benjamini Mkapa alisema Serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imesikia kilio hicho cha mtoto huyo akiomba msaada wa matibabu baada ya Mudisha tv kuripoti.

"Baada ya Serikali ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kusikia kilio cha mtoto huyu akiomba msaada wa matibabu nimeagizwa kufuatilia na sasa tumempokea saa saba usiku kuamkia Dec 26.2024 Hospitali ya Benjamin Mkapa baada ya Serikali ya Mkoa wa Manyara kumsafirisha na sasa anaendelea na matibabu yake"amesema Dr Humber.


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DED HANANG AKUTANA NA WADAU WA STAKABADHI GHALANI

DED HANANG AKUTANA NA WADAU WA STAKABADHI GHALANI Na, Mudishatv blog Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Teresia Irafay,...

Popular Post